nadharia ya sarufi zalishi



Katika kazi hii tumejadili nadharia ya sarufi zalishi ambapo tumeangalia msingi wa nadharia hii pamoja na dhana zake,pia tathmini yetu kuhusu nadhalia hii. Lakini kabla ya kuijadili nadharia hii tutaanza na kutoa maana ya istilai mbalimbali ambazo zinapatikana katika kazi hii kwa mujibu wa wataalam mbalimbali.
Massamba, (2009) anasema kuwa, nadharia ni taratibu , kanuni na misingi ambayo imejengwa katika muundo wa kimawazo kwa madhumuni ya kutumiwa kama kielelezo cha kueleza jambo.
Wafula na Njogu (2007) wanasema, nadharia ni jumla ya maelekezo yanayomsaidia msomaji au mhakiki kuifahamu kazi ya fasihi kwa kufuata utaratibu maalumu.
Hivyobasi,nadharia ni mawazo au mwongozo unaomsaidia mtu kueleza kutatua au kueleza jambo fulani.
Kihore (2005) anasema, sarufi ni sayansi ya muundo wa lugha pamoja na sheria, kanuni na matumizi yake ambayo kwa kawaida hukubalika kwa watumiaji wake.
Massamba na wenzake (1999) wanaeleza kuwa, sarufi ni kanuni na sheria au taratibu za uchambuzi zinazotawala lugha.
Hivyobasi, sarufi ni taaluma ya uchambuzi wa lugha inayojumuisha viwango vyote vya uchambuzi yaani kiwango cha umbo, kiwango cha sauti, kiwango cha miundo na kiwango cha maana.
Baada ya kuangalia maana ya dhana hizi kutoka kwa  wataalam mbalimbali.
Nadharia sarufi zalishi iliasisiwa na mwanaisimu Noam Chomsky (1928) ambaye alichapisha kitabu Syntactic structures mwaka (1957) ambapo katika kitabu hiki alizua dhana ya sarufi zalishi, ambayo ilileta mapinduzi ya msingi katika taaluma ya isimu. Mawazo ya Chomsky yalidhihirisha kuwa mbinu za uchanganuzi wa sentensi zilizotumika hapo awali hazikuwa toshelevu, hivyo sarufi zalishi ilizuka kutokana na kasoro za sarufi miundo katika uchanganuzi wa lugha.(Matinde, 2o12)
Chomsky, amewasilisha mtazamo wa Sintaksia unaotambuliwa kama Sarufi  Zalishi.Katika kazi hiyo,Chomsky alikusudia kukuza fafanuzi mwafaka za hali ya sintaksia ya lugha mbalimbali,yaani jinsi lugha mahususi zinavyounganisha maneno kuunda sentensi.Vile vile kazi hiyo ilidhamiria kukuza nadharia ya kijumla ya sintaksia inayobainisha ni mambo yapi ya kijumla yanayopatikana katika lugha mbali mbali na jinsi gani masuala hayo yanavyotofautiana katika uwanja huu wa sintaksia.
Msingi wa nadharia ya sarufi zalishi ulijikita katika uundaji wa nadharia ambayo ingeeleza namna lugha hutumiwa na watumiaji wake hasa kwa kutazama namna wanavyotumia kanuni chache zilizopo katika lugha yao kuzalisha sentensi nyingi na zisizo na kikomo, katika kurejerea hali mbalimbali, ingawa sentensi hizo zinaweza kuwa sahihi au zisizo sahihi.
( Matinde, 2012)

Dhana za msingi za nadharia sarufi zalishi;
Umilisi, huu ni ujuzi alionao mjua lugha kuhusu lugha yake. Ni ujuzi alio nao mjua lugha ambao upo katika ubongo wake. Ujuzi huo huhusu kanuni zinazotawala lugha hiyo husika. Ujuzi huu humwezesha kutambua sentensi sahihi, zisizo sahihi na kupambanua sentensi zenye utata. Ujuzi huo humwezesha kupuuza makosa ya kiutendaji katika mazungumzo kama vile kuteleza kwa ulimi, na kukatisha sentensi.
Chomsky anaeleza kuwa  mtu anapojifunza lugha huanzia na umilisi (ujuzi) na anaendelea kudai kuwa kwa kiasi kikubwa umilisi wanaokuwa nao wazawa wa lugha moja hufanana na hii ndiyo inayowafanya waelewane katika mazungumzo yao kwamba mzungumzaji anasema kile anachotaka kusema na msikilizaji anaelewa kile kilichosemwa na msikilizaji.(Rubanza,2003)
Umilisi humwezesha mzawa wa lugha:
Ø  Kuijua miundo ya sentensi katika lugha yake mfano mmilisi wa lugha ya kiswahili lazima ajue muundo wa sentensi za kiswahili kuwa unaanza na nomino,ukifuatiwa na kitenzi na kuishia na kielezi.                                    
               Mfano: Baba anaongea na mjomba.                                                                                                     Juma  amekwenda sokoni.                           
Kwa hiyo mmlisi wa lugha hawezi kuchanganya muundo huu wa sentensi za kiswahili kwa kusema;
            Mfano:   Amekwenda   Juma   sokoni.                                                                                                    Shambani   analima  baba.                  
 Kwa hiyo, kulingana na muundo wa sentensi za kiswahili, muundo wa sentensi zilizopo katika mfano wa pili si sahihi kwani zimekiuka sintaksia ya lugha Kiswahili.
Ø  kutambua sentensi sahihi na mbazo si sahihi mfano:
                 Hamis ni kijana mpole (Sahihi)
                  Mtundu mtoto ni wako (si sahihi)
Ø  Kutunga sentensi nyingi zenye urefu wowote:

Kijana mpole na mstaarabu uliyeonana nae jana, nimekutana nae leo asubuhi amekamatwa na polisi kwa tuhuma za ujambazi.

Ø  kutambua sentensi zenye utata, mfano;
              Baba Joni amefika.
              Nyumbani kwao kuna mbuzi

Ø   kutambua sentensi zenye maana sawa.
Mfano;
Watoto wapo uwanjani wanacheza mpira.
Mpira unachezwa na watoto uwanjani.

Ø   kutambua aina mbalimbali za sentensi katika lugha yake,
mfano;
Leo ni sikukuu ya mashujaa (sentensi arifu).
Njoo hapa! (sentensi amrishi)
Umenunua kalamu ngapi? (sentensi ulizi)
Kumbe umerudi! (sentensi mshangao)
Hansi angelisoma kwa bidii angelifaulu. (sentensi shurutia).
Hivyo mmilisi wa lugha huweza kuelewa sentensi hizi zinataka nini.
Ø  kutambua sentensi zenye maana na zile zisizo na maana.
Mfano;
·         Kitabu anasoma mwanafunzi.
·         Mwanafunzi anasoma kitabu.
Mmilisi wa lugha huweza kuelewa kuwa sentensi ya kwanza ni sahihi, lakini sentensi ya pili si sahihi.
 Dhana nyingine ya msingi katika nadharia ya sarufi zalishi ni utendaji, utendaji ni utumiaji wa lugha katika mazingira halisi ambao huweza kuathiri maana za maneno kulingana na matumizi yake au  mambo yanayomhusu mzungumzaji mwenyewe kama vile kutokuwa makini au kukosa kumbukumbu, kuongea akiwa amekasirika, kasoro za ala za sauti kamavile mapengo, kigugumizi na kadharika. Utendaji ni usemaji na utumizi wa ujuzi wa mzawa wa lugha katika kutumia lugha yake ndani ya muktadha mahususi, mtumiaji wa lugha huweza kuitumia lugha kulingana na mazingira aliyopo. Matumizi ya lugha huzingatia muktadha, wahusika, jinsia, utamaduni na mada ya mazungumzo.  (Yule, G. 1997).
Mfano:
·         Muktadha:
                            Muktadha wa stendi    -    Kula vichwa.
                Muktadha wa hotelini  -   nipe wali kuku.
                 Muktadha wa kanisani -  Bwana awe nanyi.

·         Wahusika
matumizi ya lugha huzingatia wahusika, kuna matumizi tofauti ya lugha kutegemeana na kundi la wahusika. Kundi la rika moja hutumia lugha inayofanana mfano kundi la vijana hutumia misemo kama;
             Twende tukale bata
 Leo Unaniachaje?
Kundi la watu wenye rika tofauti huwa na matumizi tofauti ya lugha.
Mfano;
Mzazi na mtoto
              Mzazi:  Mwanangu niletee kikoi changu.
              Mtoto: Sawa mama.
Mwajiri na mwajiriwa.
              Mwajiri    :  Leta faili la madai.
              Mwajiriwa:  sawa mkuu.
Mada ya mazungumzo
Mada za mazungumzo zipo nyingi, Kuna mada za kijamii, kwa mfano ndoa, unyago, mapenzi, kifo, matanga, burudani na muziki  Kuna mada za kibiashara kwa mfano bidhaa, kodi, vibali, fedha, hasara na faida.  Kwa hiyo, ili mazungumzo yaweze kwenda vizuri, wazungumzaji wanatakiwa kuzingatia mada husika.
Mfano: wafanyabiashara
               Mzigo mpya umeingia.
               Nauza vocha kwa bei ya jumla.
Mada ya kilimo
                   Mbolea ya ruzuku bado haijaletwa.
                    Mwaka huu nitawahi kupalilia shamba.
Dhana nyingine ya nadharia ya sarufi zalishi ni umbo la ndani, umbo hili hujitokeza katika sentensi kabla ya sentensi hiyo kufanyiwa mageuzi yoyote. Umbo la ndani hubeba maana kamili ya tungo na vipashio vya tungo hubainika bayana kwani huwa havijafanyiwa mageuzi yoyote.
Mfano sentensi zifuatazo zipo katika umbo la ndani
                    Amina piga mtoto kila siku
                    Shida anunua chumvi kwa mangi
                     Mama enda shambani asubuhi.
                      Mpendi wangu amerudi
Umbo la nje, umbo hili hutokea baada ya umbo la ndani kufanyiwa mageuzi muhimu hadi kufikia kiwango cha usemaji sahihi na unaokubalika. Umbo la nje hudhihirika kimatamshi na kiothografia, yani umbo hili hutamkika na kuandikika.
 
 Mfano;   Amina humpiga mtoto kila siku
                 Shida amenunua chumvi kwa Mangi.
                 Mama ameenda shambani asubuhi.                       
                  Mpenzi wangu amerudi.
Dhana ya mwisho ya sarufi zarufi  ni uchamko, chamko ni utaratibu wa kutumia sheria fulani ambazo huweza kutumika mara kwa mara katika kuunda sentensi ambazo zina urefu usio na kikomo . uchamko hutokana na sentensi zaidi ya moja kupachikwa katika Sentensi ile ya kwanza ili kuunda sentensi moja isiyo na kikomo, pia hutumia kanuni chache kutunga sentensi nyingi zisizo na kikomo. Uchamko umegawanyika katika sehemu mbili yaani utegemezi na uambatanishaji.
Utegemezi
Ni uchamko ambao hutokana na hali ya kuwepo au kutokuwepo kipashio kimoja cha kiisimu ambacho kinategemea uwepo wa kipashio kingine. Utegemezi hutambulishwa na maneno kama vile; ili, kwamba, kama na kuwa. (Matinde, 2012)
 Mfano; Ambakisye alijua kuwa Ndope anafahamu kuwa shule itafunga kesho.
              Asha anajua kuwa mimi najua kuwa atafaulu mtihani.
Uambatanishaji.
Ni aina ya uchamko ambao hudhihirishwa na uambatishaji wa sentensi sahili mbili au zaidi. Kwahiyo, huu ni uchamko ambao hutokana na sentensi ambatano.
Mfano;  Shangazi anapika, mama anaandaa chakula na baba anakula.




                                             


 

                                         S

                         KN                             KT

         N                                   T                                          S2

 Shangazi                         anapika                     KN                                         KT

                                                                          N                              T            U               S3

                                                                      Mama                    anaandaa      na      KN        KT
                                                                                                                               
                                                                                                                                 N             T

                                                                                                                            Baba     anakula




Kama ilivyo kwa nadharia zingine nadharia hii pia ina ubora na udhaifu wake.
Ubora wa nadharia hii.
·         Imeweza kuonesha umilisi alionao binadamu katika lugha yake, kuwa anaweza kuzalisha tungo au sentensi mbalimbali kwa kutumia kanuni chache zilizopo katika lugha yake.Umilisi huo humsaidia mtumiaji wa lugha kuunda sentensi hizo hata kama hajui kusoma na kuandika.
·         Pia nadharia hii inaonesha kuwa kila mzungumzaji wa lugha huzifahamu vizuri kanuni chache zilizopo katika lugha yake na kuzitumia kanuni hizi katika kuwasiliana na jamii inayomzunguka.
·         Vilevile nadharia hii ya sarufi zalishi imeweza kuonesha kuwa binadamu anao uwezo wa kufafanua kipi ni sahihi na kipi sio sahihi katika uteuzi wa maneno wakati wa uzungumzaji.
·         Nadharia hii inamchukulia binadamu kama kiumbe chenye uwezo endelevu wa kuzalisha sentensi ambayo inaweza kueleweka kwa jamii inayomzunguka.
·         Pia nadharia inatuonesha kwamba upo uhusiano mkubwa kati ya akili, kufikili na lugha.Hususan katika dhana ya utendaji mtumiaji wa lugha anatakiwa kutumia akili anapoteua lugha ya kutumia ili kuendana nas muktadha.
Udhaifu wa nadharia hii.
·         Inafafanua namna au jinsi watu wanavyozungumza lugha na sio kuwaeleza wazungumze vipoi lugha hiyo.
·         Haitilii mkazo mabadiliko katika lugha hata kama yapo.
·         Vipengele kama umbo la ndani na umbo la nje vinaweza kumchanganya mtu anaejifunza lugha.
Hivyo ni kweli kwamba nadharia ya sarufi zalishi imeleta mapinduzi makubwa katika taaluma ya sarufi miundo.


Comments

  1. Nina swali,huku ukitoa mifano,fafanua majukumu ya nomino katika nadharia ya semantiki zalishi

    ReplyDelete
  2. fafanua jinsi ferdinand de saussure alivyochangiakatika taaluma ya isimu

    ReplyDelete
  3. Nashukuru kwa hii dondoo ya sarufi zalishi. Je ni zipi sheria za uchamko?

    ReplyDelete
  4. Dhana ya mofimu kabla ya sarufi zalishi

    ReplyDelete
  5. Sifa za mofimu kabla ya sarufi zalishi ni zipi?

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

notes za malenga wapya,uhakiki wa shairi la malenga wapya.

Semantiki kama taaluma nyingine ina mahusiano na taauma nyingine kama ifuatavyo katika mchoro na hatimaye katika maelezo yanayo eleza vipengele mbalimbali vya lugha:-

maana ya sintaksia,uhusiano wa sintaksia na matawi mengine,malengo ya sintaksia au isimu miundo, vipashio vya lugha ni vipi?,